Jinsi ya Kujisajili Kwenye AQRB
Bodi inatambua aina mbalimbali za wataalamu na wanafunzi. Usajili unategemea hadhi ya muombaji:
|
Hadhi |
Maelezo ya Usajili |
|
Mwanafunzi / Mhituumu (Graduate) |
Kwa mhitimu wa shahada inayotambuliwa katika Ubunifu Majengo, Ukadiriaji Majenzi au taaluma zinazohusiana. Wanaweza kuanza usajili kama Graduate ili kupata uthibitisho wa kuanza mafunzo ya vitendo-AQIP |
|
Mtaalamu (Professional) |
Muombaji lazima awe tayari amesajiliwa kama Graduate na kuwa na uzoefu wa vitendo wa taaluma-AQIP chini ya mtaalamu aliyesajiliwa. Baada ya kuthibitishwa na kufaulu mitihani, atasajiliwa rasmi kama Mtaalamu. |
|
Technician |
Kwa wahitimu wa kozi za ufundi zinazotambulika, wanaweza kujisajili kama Technician. Hii inawapa heshima ya kitaaluma na kuwezesha kushiriki kwenye miradi chini ya usimamizi wa mtaalamu. |
|
Draughtsman |
Kwa wahitimu wa kozi za uchoraji wa usanifu na mbinu za ujenzi. Usajili huu unasaidia kuzingatia viwango vya kitaaluma na kazi salama za uchoraji na mbinu za ujenzi. |
Hatua za Jumla za Usajili
- Kukidhi sifa za taaluma kulingana na hadhi.
- Kuandaa nyaraka muhimu (vyeti, transcripts, kitambulisho, picha ndogo, uthibitisho wa uzoefu).
- Kujaza fomu ya maombi mtandaoni kupitia mfumo rasmi wa AQRB-ORS
- Kulipa ada husika.
- Kuthibitishwa na kuingizwa kwenye rejista rasmi kulingana na hadhi