Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Ujenzi

Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi

Hatimiliki

Karibu kwenye tovuti yetu. Kwa kuendelea kuvinjari na kutumia tovuti hii, unakubali kufuata na kushikamana na sheria na masharti yafuatayo ya matumizi. Sheria hizi, pamoja na sera yetu ya faragha, zinatawala uhusiano wako na Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) kuhusiana na tovuti hii. Ikiwa hukubaliani na sehemu yoyote ya masharti haya, tafadhali usitumie tovuti hii.

Neno AQRB, “sisi” au “bodi” linamaanisha mmiliki na msimamizi wa tovuti hii, yaani Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi, Tanzania. Neno “wewe” linamaanisha mtumiaji au mtembeleaji wa tovuti hii.

Matumizi ya tovuti hii yanategemea masharti yafuatayo:

  1. Matumizi kwa Jumla
    Maudhui ya kurasa za tovuti hii ni kwa taarifa za jumla na matumizi tu. Maudhui haya yanaweza kubadilishwa bila taarifa ya awali.

  2. Hakuna Udhamini
    Hatuwezi, wala wahusika wengine, kutoa udhamini wowote au hakikisho kuhusu usahihi, wakati, utendaji, ukamilifu, au unafaa wa taarifa na nyaraka zilizopo kwenye tovuti hii kwa madhumuni yoyote maalum. Unatambua kuwa taarifa na nyaraka hizi zinaweza kuwa na makosa au upungufu, na tunatoa kielelezo cha kutokuwa na dhima kwa makosa hayo kadiri inavyokubaliwa na sheria.

  3. Matumizi Kwa Hatari Yako
    Matumizi yako ya taarifa au nyaraka zozote kwenye tovuti hii ni kwa hatari yako mwenyewe. Ni jukumu lako kuhakikisha kuwa bidhaa, huduma, au taarifa zilizopo kwenye tovuti hii zinakidhi mahitaji yako maalum.

  4. Haki za Kiakili
    Tovuti hii ina nyaraka ambazo ni mali ya AQRB au zimeruhusiwa kwa AQRB. Hii ni pamoja na, lakini siyo tu, muundo, mpangilio, sura, na michoro. Kurudia nyaraka hizi kinyume na ilivyoelezwa kwenye hakimiliki kunakatazwa.

  5. Alama za Biashara
    Alama zote za biashara zilizotumika kwenye tovuti hii ambazo sio mali ya AQRB au ruhusiwa kwa AQRB, zimetambuliwa kwenye tovuti.

  6. Matumizi Yasiyoruhusiwa
    Matumizi yasiyoruhusiwa ya tovuti hii yanaweza kusababisha madai ya fidia na/au kuwa kosa la jinai.

  7. Viungo vya Nje
    Mara kwa mara, tovuti hii inaweza kujumuisha viungo vya tovuti nyingine. Viungo hivi vimewekwa kwa urahisi wako na kupata taarifa zaidi. Viungo hivi havimaanishi kuwa tunathibitisha au kuunga mkono tovuti hizo. Hatuna dhima kwa maudhui ya tovuti hizo zilizounganishwa.

  8. Sheria Zinazotumika
    Matumizi yako ya tovuti hii, na mzozo wowote unaotokea kutokana na matumizi hayo, yanatawaliwa na sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.